Nguvu za Kukaa

Nguvu za Kukaa

Tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu… WAEBRANIA 12:2

Watu wanaomaliza vizuri maishani ni wale walio na tabia thabiti. Kama waaminio, tunaweza kuwa wenye shukrani kwamba Roho Mtakatifu anajenga tabia ndani yetu kwamba tunahitaji kufanya kile Mungu anatuita tufanye—tuna “nguvu za kukaa.” Yesu hakukata tamaa hali zake zilipokuwa ngumu, na Yeye ndiye mfano wetu. Biblia inasema tusitazame yote yanayotuondoa njiani badala yake tumtazame Yesu.

Ninafikiri wengi wetu tunataka kufanya na kuwa kila kitu ambacho Mungu alikusudia kwa ajili yetu, na kukifurahia safarini. Furaha kuu huja baada ya kukamilisha mwendo ambao Mungu amekuita kutembea. Furahia safari na utie macho yako kwenye thawabu. Mojawapo ya ushuhuda unaoweza kuwa nao ni bado ningali hapa. Unaposema maneno hayo, unasema, “Sikukata tamaa. Sikuvunjika moyo. Bado ningali hapa.”


Sala ya Shukrani

Baba, ninakushukuru kuwa, kwa usaidizi wa Roho Mtakatifu, nina nguvu za kukaa. Ninafanya uamuzi leo wa kuendelea—kutokata tamaa. Nisaidie kukimbia mbio zangu kwa uvumilivu na kutambua furaha ya kumaliza kila kazi vizuri.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon