Basi, kwa njia yake yeye, na tumpe Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani, tunda la midomo iliungamanayo jina lake. WAEBRANIA 13:15
Watu wengi wamezoea maelezo, “Kuna nguvu katika sifa!” Ni kweli, na tunapomsifu Mungu kutoka kwa mioyo yetu, tunashinikiza nguvu katika ulimwengu wa kiroho. Mungu mwenyewe huketi juu ya sifa za watu wake (tazama Zaburi 22:3).
Sifa huturuhusu kukumbuka na kuonyesha furaha na shukrani zetu kwa yote ambayo Mungu ametutendea…na kile kitu ambacho atafanya. Inashirikisha mioyo yetu kumwelekea na midomo yetu kuongea kumhusu.
Shukuru kuwa, tunaweza kufyonza ndani ya nguvu ambazo huachiliwa kupitia kwa sifa—inatupatia nafasi ya kuonyesha vile kweli tulivyo na shukrani. Tunafanya hivi kwa sababu tunampenda Mungu, lakini pia kwa sababu sifa na shukrani ni nia ambazo Mungu hufurahia. Kuomba kwa shukrani ndiyo njia ya kuona maombi yakijibiwa.
Sala ya Shukrani
Baba, ninakushukuru kwa sababu unastahili kusifiwa. Asante kwa kila kitu ambacho umefanya katika maisha yangu na kila kitu utakachofanya katika siku zijazo. Ninakupenda na kukusifu pamoja na vitu vyote nilivyo navyo.