
Maana, sasa je! Ni wanadamu ninaowashawishi, au Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa hata sasa nawapendeza wanadamu, singekuwa mtumwa wa Kristo. Wagalatia 1:10
Je, wewe ni mtu ambaye Mungu alikuumba kuwa au unaishi “kufurahisha watu”? Kwa mujibu wa maandiko haya, mapenzi ya Mungu ni kwa ajili yetu kumpendeza na kuwa kile anataka tuwe.
Unapochagua kuwa mtu ambaye Mungu alikuumba kuwa wa kipekee na tofauti kuliko kila mtu mwingine – unatarajia kuteswa. Haitakuwa rahisi kukabiliana nayo kila wakati, lakini huwezi kujipenda sana ikiwa unapingana na imani zako mwenyewe.
Tazama, kuenda pamoja na umati, unapojua moyoni mwako kwamba Mungu ndiye anayekuongoza kwa njia tofauti, ni sababu moja ya kufanya watu wasifanikiwe kuwa wao wenyewe.
Ninataka kukuhimiza uende nje na uwe mtu ambaye Mungu alikufanya uwe. Usiruhusu njia ya mtu mwingine au jinsi anakuchukulia kuamua thamani yako. Kuwa na ujasiri wa kuwa tofauti na kushughulika na upinzani. Kumbuka kwamba Mungu anakukubali na anakupenda. Alikufanya uwe jinsi ulivyo kwa sababu, na una kitu maalum cha kutoa.
OMBI LA KUANZA SIKU
Mungu, sitaki kuishi nikijaribu kuwafurahisha wanadamu. Ninatamani kuwa tofauti. Nataka kuishi na neema yako na kuwa mtu ambaye ulinifanya kuwa.