Bali sasa tumefunguliwa katika torati, tumeifia hali ile iliyotupinga, ili sisi tupate kutumika katika hali mpya ya roho, si katika hali ya zamani, ya andiko. Warumi 7:6
Ninaamini mojawapo ya sababu kubwa ambazo watu wengi wanachoshwa na kuvunjika moyo ni kwa sababu wanaenda kwa njia yao wenyewe badala ya kufuata mpango wa Mungu.
Tunahitaji kufuata uongozi wa Roho Mtakatifu kuhusu kile tunachopaswa kushiriki na ambapo tunapaswa kutumia nguvu zetu. Lazima tujifunze kusema ndiyo wakati anasema ndiyo na hapana wakati anasema hapana. Tunapotii mwongozo wa Mungu, tutaweza kukamilisha kile anachotupa kufanya na kutembea kwa amani. Warumi 7: 6 inasema tunapaswa kuongozwa na “kuhamasishwa kwa Roho.” Naweza kukumbuka nyakati nyingi wakati nilikuwa nimechoka na Roho Mtakatifu aliniamuru kupumzika, lakini niliendelea kushinikiza mwenyewe kwenda nje au kuwa na watu wengine . Kisha nilidhoofika mno badala ya kuchoka tu. Kama unavyojua, watu wenye kuchoka hukosa starehe na subira.
Tunapotii ushawishi wa Roho Mtakatifu, Yesu huinuliwa. Basi napenda kukuuliza hivi: Je! Umechoka … au Yesu ameinuliwa? Fuata Roho na kumtukuza katika maisha yako.
OMBI LA KUANZA SIKU
Mungu, sitaki kuwa nimechoka sana nikose kutii mwitikio wako. Ninaamua kufuata mipango yako na kukuinua katika maisha yangu.