Tazama, jinsi ilivyo vyema, na kupendeza, ndugu wakae pamoja, kwa umoja! ZABURI 133:1
Kubishanabishana kati ya watu wa Mungu si jambo jipya. Ilikuwa shida katika kanisa la kwanza, vile tu ilivyo sasa. Paulo alilihimiza na kulisihi sana kanisa kuwa na umoja na akaandika katika Wafilipi 2:2: “Ijalizeni furaha yangu, ili muwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja.”
Panapokuwa na umoja, panakuwa na baraka na upako. Watu wanaposhukuru kwa ajili ya kila mmoja wao na kuchagua kuishi katika umoja, watashuhudia nguvu za makubaliano. Lakini nguvu za Mungu haziwezi kufanya kazi katika maisha yetu tukiwa na uchungu na kuwasirikia watu. Upendo wake hauwezi kutiririka kupitia kwetu ikiwa tunashikilia ugomvi na chuki. Amani ni sawasawa na nguvu, na kutokuwepo kwa amani ni sawasawa na kukosa nguvu.
Sala ya Shukrani
Ninakushukuru leo, Baba, kwa nguvu tunazokuwa nazo tunapoamua kuja pamoja katika umoja. Leo ninaamua kuweka ugomvi kando na mabishano ili kufuatilia amani na umoja. Ninashukuru kwamba utanisaidia kufanya hivi katika nguvu zako.