Tegemeo katika Mungu Peke Yake

Tegemeo katika Mungu Peke Yake

Hawa wanataja magari na hawa farasi, bali sisi tutalitaja jina la Bwana, Mungu wetu. —ZABURI 20:7

Ili kufanikiwa katika jambo lolote, ni muhimu kuwa na tumaini, lakini cha kwanza kabisa, lazima liwe tumaini ndani ya Mungu na ahadi zake, siyo kutumainia kitu kingine chochote. Kama waaminio, tunaweza kuwa na tumaini ndani ya upendo wa Mungu, wema na rehema zake. Hili tumaini linatuhakikishia ya kwamba Baba yetu wa mbinguni anataka tufaulu.

Mungu hakutuumba ili tushindwe. Tunaweza kushindwa katika mambo mengine njia ya kuelekea mafanikio, lakini tukimtumainia, atachukua hata makosa yetu na kuyabadilisha kuwa mema kwa ajili yetu (Warumi 8:28).

Waebrania 3:6 inatuambia “…kama tukishikamana sana na ujasiri wetu na fahari ya taraja letu mpaka mwisho[Kristo].” Ni muhimu kutambua kwamba, makosa sio mwisho wa mambo tukishikilia tumaini letu.

Kila mmoja wetu ana kusudi, lakini kwa kuwa tu tumekusudiwa kufanya kitu, haimaanishi kwamba kitafanyika chenyewe. Nilipitia mambo mengi sana Mungu alipokuwa akinikuza pamoja na huduma yangu. Kuna nyakati ambazo nilikaribia kupoteza tumaini langu kuhusu mwito uliokuwa juu ya maisha yangu. Ilibidi nimtegemee Bwana kila wakati na kuweka tumaini langu ndani yake kabla nisonge mbele tena. Jambo hilo ni kweli kukuhusu. Ukijaribiwa kupoteza tumaini lako, mkaribie Mungu na uweke tumaini lako ndani yake.


Tia tumaini lako ndani ya Mungu peke yake, na atakusababisha kufanikiwa kwa kweli.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon