
Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli. 2 TIMOTHEO 2:15 BIBLIA
Tunaweza kujitahidi kutenda mema kwa ajili ya Mungu, lakini hatuwezi kumpa utimilifu, na hatuhitaji kuhisi kwamba tunashinikizwa kufanya hivyo.
Nilisikia kisa kuhusu mwanafunzi ambaye alimgeuzia profesa wake makala na profesa akaandika chini yake, “Je, hivi ndivyo unavyoweza kujitahidi zaidi?” Akijua kwamba hazikuwa jitahada zake zote, mwanafunzi huyo akaandika upya makala, na mara kwa nyingine tena, profesa akamrudishia na kifungu hicho hicho chini ya makala. Hili liliendelea mara tatu na mwishowe profesa alipouliza iwapo aliandika kwa jitihada zake zote, alifikiri kwa muda wa dakika moja na akajibu, “Ndiyo, ninaamini niliandika kwa jitihada zangu zote.” Halafu profesa akasema, “Sawa, sasa nitaikubali.”
Vile vyote Mungu anataka ni kile chetu kizuri sana—anaweza kufanya kazi nacho. Tunaweza kushukuru kwamba hata kama kizuri chetu sio kitimilifu, Mungu anaweza kufanya kitu kitimilifu cha ajabu nacho!
Sala ya Shukrani
Baba, ninashukuru kwamba unapendezwa nikitia jitihada zangu zote kwa ajili yako, hata ingawa kizuri changu kiko mbali na kitimilifu changu. Asante kwa kuwa ninapofanya sehemu yangu, huwa unakuwa mwaminifu halafu unafanya sehemu yako na maisha yangu.