Acha Mungu Akuongoze Katika Maisha

Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana, basi chagua uzima (KUMBUKUMBU LA TORATI 30:19)

Katika Yohana 16:8, Yesu alisema Roho Mtakatifu “atathibitisha na kushawishi” ulimwengu kuhusu dhambi na haki. Hakusema lolote kuhusu Roho Mtakatifu kuleta hukumu. Alisema analeta “thibitisho… kuhusu dhambi na haki.”

Roho Mtakatifu hufunua matokeo ya dhambi na matokeo ya haki ndipo watu waelewe njia watakayofuata. Anatofautisha wazi kati ya mema na mabaya, kati ya baraka na laana, kati ya uhai na mauti ili watu wamwombe Mungu kuwasaidia kuchagua uhai.

Watu ambao wanaishi katika dhambi wana maisha ya ufukara na dhiki. Wakati mwingine huwa ninakutana na watu niliojua miaka mingi iliyopita na ambao sijawahi kuona muda mrefu. Baadhi ya watu hawa wamekuwa hawamwishii Mungu na mienendo ya maisha migumu na yenye miparuzo waliochagua imewadhoofisha. Uteuzi mchachu, wenye huzuni, na dhiki waliofanya unaonekana kwa sababu dhambi imewaacha wakiwa wenye huzuni na kuonekana wazee kuliko vile walivyo. Hawana furaha, wana mielekeo chanya, na watu wasiokuwa na ridhaa waliojawa uchungu kwa sababu maisha yamekuwa mabaya. Wanakosa kugundua kwamba maisha yao ni matokeo ya uteuzi mbaya waliofanya.

Matokeo ya dhambi yanaweza kuonekana kila mahali. Mpaka kati ya wanaompenda na kumtumikia Mungu na wale waisompenda na kumtumikia imeanza kuwa dhahiri sana. Mungu hutuomba kufanya uteuzi mzuri, ambao utatuongoza katika maisha anayotamani tufurahie. Kuna njia mbili mbele zetu: njia pana inayotuongoza katika dhambi na uharibifu na njia nyembamba inayotuongoza katika uzima (soma Mathayo 7:13-14). Ninakuhimiza kuchagua uzima leo na kila siku.

NENO LA MUNGU KWAKO LEO:

Uteuzi mzuri huja kuwa maisha mazuri.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon