Hatua Moja Kwa Wakati

. . . Yeye aliyeanzisha kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu… —Wafilipi 1:6

Ninapozungumza kuhusu uponyaji wa vidonda vya kihisia, ningependa kuinua nyuzi za viatu zenye rangi nyingi zilizofungwa pamoja kwa kifundo. Ninaiambia hadhira, “Hivi ndivyo unavyoanza mchakato wa kwanza wa mabadiliko na Mungu. Huwa umefundika. Kila kifundo kinawakilisha shida tofauti katika maisha yako ambayo imekua kutokana na mambo uliyopitia. Huenda kufungua vifundo hivyo na kunyosha shida hizo kukachukua muda kidogo na bidii, kwa hivyo usivunjike moyo iwapo haitafanyika mara moja.”

Ukitaka kupokea uponyaji na kuja katika eneo la ukamilifu, lazima utambue kwamba uponyaji ni mchakato. Ruhusu Mungu kukushughulikia pamoja na shida zako kwa njia yake na kwa wakati wake. Kazi yako ni kushirikiana naye katika kila eneo analochagua kuanza nalo.

Katika jamii yetu ya sasa ambapo mambo hufanywa haraka, huwa tunatarajia kila kitu kufanyika haraka na kwa urahisi. Bwana huwa hana haraka, na huwa hakati tamaa. Wakati mwingine inaweza kuonekana kwamba hupigi hatua yoyote. Hiyo ni kwa sababu Mungu anafungua kila kimoja cha vifundo vyako kwa wakati mmoja. Mchakato huu unapoendelea, tunajifunza kumwamini Mungu, na kukuza uhusiano wa karibu na wa ndani naye. Daima Mungu hukamilisha, alichoanzisha, na utaona uhuru na ushindi katika maisha yako!


Usikate tamaa!

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon