Irudieni ngome, enyi wafungwa wa tumaini; hata hivi leo nasema ya kwamba nitakurudishia maradufu. Zakaria 9:12
Nina swali kwako: Unatarajia nini? Unatarajia nini katika maisha? Je! Unatafuta kitu kizuri cha kutokea au unatarajia kukata tamaa?
Watu wengi wanahisi kukata tamaa siku hizi. Hata hivyo, Yesu hakufa kwa ajili yetu kukosa tumaini. Alikufa ili tuweze kuwa na tumaini. Ibilisi anataka kuiba tumaini lako, naye atakuambia uongo.
Atakuambia kuwa hakuna jambo lolote linaloweza kutokea katika maisha yako au kwamba mambo mema unayoyajali hayataendelea. Ikiwa unakabiliwa na hali ngumu, atakuambia kuwa haitaisha kamwe. Lakini endelea katika tumaini na kumbuka kwamba shetani ni mwongo.
Mungu anaweza kubadilisha kila kitu! Baba yetu ni mzuri, na ana mpango mwema kwa maisha yako. Ikiwa utakuwa na tumaini lako, hasa katikati ya nyakati za wasiwasi na zisizo na uhakika, amekuahidi “mara dufu kwa shida yako.” Kwa hiyo kataa kukosa tumaini. Anza kutarajia Mungu kufanya kitu – kitu kizuri!
OMBI LA KUANZA SIKU
Bwana, tumaini langu liko kwako. Shetani ni mwongo nami sitamsikiliza kisha nipoteze tumaini. Ninakutarajia kutenda jambo jipya maishani mwangu.