Mkaribie Yeye

Mkaribie Yeye

Huyo Roho akaaye ndani yetu hututamani kiasi cha kuona wivu? Yakobo 4:5

Je! Unataka kuwa karibu na Mungu? Anataka kuwa karibu na sisi. Andiko hapo juu linasema Roho Wake anakaa ndani yetu na anatamani kuwakaribisha kwa upendo kiasi cha kuona wivu. Kwa hiyo unaweza kuwa karibu kiasi gani?

Tunaweza daima kukaribia katika uhusiano wetu na Mungu. Kwa kweli, sisi ndio ambao tunaamua jinsi tu uhusiano wetu pamoja Naye utakuwa. Hata ingawa anaishi ndani yetu, Roho Mtakatifu hatalazimisha uhusiano na sisi. Anataka tupate kumkaribisha katika maisha yetu.

Mungu alituumba kwa ajili ya ushirika na anatamani sana uhusiano na sisi. Anatamani kuzungumza na sisi, kutusikiliza, kutufundisha na kutuongoza-yaani kuwa sehemu ya maisha yetu. Na sisi ni bora kwa hilo! Tunafanywa upya wakati tunashirikiana na Mungu.

Faida za kutumia muda na Baba hazina mwisho. Rafiki zangu, nawahimiza kuwa na msimamo katika kutenga wakati wa ushirika na Baba. Anasubiri. Anasema, “Njoo kwangu …” Kwa hiyo endelea … na uone kile kilichohifadhiwa!

OMBI LA KUANZA SIKU

Mungu, inanishangaza  jinsi unavyotaka ushirika na mimi. Ninataka kuwa karibu na Wewe pia. Asante kwa kunipenda na kunikaribia wakati ninapokukaribia.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon