Kuwa Yule ambaye Mungu anatafuta

Kuwa Yule ambaye Mungu anatafuta

Kwa maana macho ya Bwana hukimbia-kimbia duniani mwote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao, waliokamilika moyo kuelekea kwake. 2 Mambo ya nyakati 16:9

Mungu anatafuta watu ambao wanapenda sana mambo anayopenda. Anatafuta watu ambao watamfuata kwa moyo wote. Anatafuta watu ambao watawapenda watu katika kazi zao, katika vitongoji na nyumba zao; wale ambao wamejitolea kupenda waliopotea, maskini na wale wanaohitaji. Anatafuta wale ambao tayari kuanza kufanya kile Biblia inatuambia kufanya.

2 Mambo ya Nyakati 16: 9 inasema kwamba Mungu daima anajitahidi kujionyesha Mwenye nguvu kwa ajili ya wale ambao nyoyo zao hazina hatia kwake Yeye.

Je, wewe ni mmoja wa watu hao? Ikiwa sio, nataka kukuhimiza na kukujulisha kwamba unaweza kuwa mtu huyo ambaye Mungu hutafuta.

Ikiwa umemjua Bwana kwa miaka mingi au umeanza maisha yako mapya ndani yake, unaweza kuwa mtu huyo ambaye atakayemtafuta Mungu na kumsikiliza Roho Mtakatifu.

Unaweza kuwa mtu huyo ambaye anaweza kufanya tofauti katika maisha ya watu wanaoumia. Leo, simama na uwe mtu ambaye Mungu anataka uwe.

OMBI LA KUANZA SIKU

Mungu, zaidi ya chochote, nataka kuwa  mtu ambaye Wewe unatafuta ulimwenguni. Nielekeze kwa njia unayotaka niende, na kunifanya ndani kuwa mtu anayewapenda wengine, anayetii Neno lako, na anayekujua kwa kweli.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon