Neno Moja nimelitaka kwa Bwana, Nalo ndilo nitakalolitafuta, Nikae nyumbani mwa Bwana Siku zote za maisha yangu, Zaburi 27:4
Maisha hayapaswi kuwa ngumu. Yesu hakufa ili tuweze kuishi maisha magumu, yaliyofadhaika,na yenye kusikitisha. Yohana 10:10 inasema Yeye alikufa kwa ajili yetu ili tuweze kufurahia maisha. Kila dakika mambo yanapokuwa magumu, kunasababisha huzuni. Tunahitaji kujifunza jinsi ya kuacha kusisitiza na kuacha kuishi maisha yenye mambo mengi.
Maisha tofauti ya kuishi ni ya urahisi. Urahisi hapa inamaanisha “moja, yenye kitu kimoja, bila kuchanganya.” Mungu ameshughulika nami juu ya kuishi maisha rahisi. Ananionyeshea kwamba njia pekee ya kufanya hivyo ni kusalia na “kitu kimoja.”
Mungu anataka sisi tuweke akili zetu kwake. Anatuambia katika Neno Lake kwamba hatuwezi kurithi Ufalme Wake kama hatuji kwake tu kama mtoto mdogo na kusema, “Naamini.”
Hiyo karibu inaonekana rahisi sana, na unaweza kutaka kuifanya … lakini sivyo! Mpango wa Mungu kwa ajili yako ni rahisi. Inaweza kuwa haina maana kwa akili yako, lakini hakuna kitu cha kukanganya na Mungu, na hataki uwe na kujichanganya. Njoo Kwake leo, ukisema, “Ninaamini.” Wacha awe “Neno moja.”
OMBI LA KUANZA SIKU
Mungu, ninakuamini. Sitaki kuishi na mzigo wa matatizo, hivyo leo, ninatafuta maisha rahisi kwa kukufanya “Kitu kimoja” ambacho ninachotafuta. Niongoze katika mpango wako rahisi kwa ajili yangu.