Kuishi katika Wakati Uliopo…na Kuupenda

Kuishi katika Wakati Uliopo…na Kuupenda

Msiyakumbuke mambo ya kwanza, wala msiyatafakari mambo ya zamani. Isaya 43:18 Biblia

Mojawapo ya vitu vizuri kuhusu maisha ndani ya Yesu ni kwamba kila siku ni mwanzo mpya—mwanzo wa kuburudisha. Hatuhitaji kujuta ya jana au kuogopa kesho. Tunaweza kusherehekea leo, tukishukuru kwa sababu ya uwepo wa Mungu tulio nao wakati huu.

Kuna msemo ninaopenda ambao husema hivi: “Jana ni historia. Kesho ni siri. Leo ni kipaji; ndiyo kwa sababu inaitwa katika Kiingereza, the present (kipaji).”

Tunaweza kufurahia kila dakika ya maisha yetu na kuishi katika wakati uliopo. Hatufai kutafakari mambo ya zamani au kutazama mbali sana ndani ya mustakabali, lakini tunahitaji kutambua wakati uliopo ni kipaji cha Mungu kwetu sisi sasa hivi. Acha tufanye uamuzi wa kushukuru kwa ajili ya leo, tuishi kikamilifu na kufurahia kila sehemu yake!


Sala ya Shukrani

Baba, asante kwa kipaji cha leo. Licha ya shida zangu za zamani au changamoto zijazo, ninachagua kusherehekea maisha yangu nawe katika wakati uliopo. Asante kwa kuwa hii ni siku uliyofanya; nitafurahi na kufurahia ndani yake.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon