Kujenga Tumaini

Kujenga Tumaini

Mtumainini Bwana siku zote maana Bwana Yehova ni mwamba wa milele. —ISAYA 26:4

Ni mara ngapi tumeruhusu hali za majaribu zinazotukabili kutusikitisha na kutuudhi bila sababu ya kuwa hivyo? Tumeishi miaka mingapi ya maisha yetu tukisema, “Oh, ninamwamini Mungu. Ninamtumainia Mungu,” ilhali kusema ukweli tukiwa tuna wasiwasi na kuzungumza vibaya, na kujaribu kuwaza tutakavyofanya bila kumhusisha Mungu?

Wakati mwingine huwa tunafikiri tunamwamini Mungu tu kwa sababu tunasema maneno, lakini ndani tuna fadhaa na mshtuko. Ni vizuri tuchukue hatua za kwanza za kumtumainia Mungu, lakini pia lazima tugundue kwamba tunaweza bado kukua katika tumaini. Kumtumainia Mungu ni zaidi tu ya maneno—ni maneno, nia na matendo.

Tumaini na hakika hujengwa kwa kipindi cha muda mrefu. Mara nyingi huchukua muda kushinda desturi iliokolea ya wasiwasi, fadhaa au hofu. Ndiyo kwa sababu ni muhimu “kuning’inia hapo ndani” na Mungu. Usiache na kukata tamaa, kwa sababu huwa unapata tajriba na nguvu za kiroho unapopitia hali tofauti. Kila wakati unakuwa na nguvu kuliko vile ulivyokuwa wakati uliopita. unakuwa na nguvu kidogo ile ulikuwa nayo wakati uliyopita.

Hivi karibuni au baadaye, usipokata tamaa, utajipata mahali pa utulivu, amani, na tumaini ndani ya Mungu.


Ukiwa katika wakati wa majaribu, gundua kwamba wasiwasi hauna maana kabisa, na utumie wakati huo kujenga tumaini lako ndani ya Mungu.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon