Mipaka ina makusudi

Mipaka ina makusudi

Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako. —Mithali 3:5-6

Kukuwa na kiasi na kujidhibiti, na kuanzisha mipaka dhabiti katika maisha yetu ni baadhi ya mambo muhimu tunayoweza kufanya. Uhai ambao hauna nidhamu ni moja ambao imejazwa na kutojali.

Neno la Mungu linaweka mipaka muhimu ili kutuweka katika eneo la usalama wa Mungu. Linatuambia nini tunaweza kufanya, na kile si bora kufanya, ili kuwa salama.

Kama Wakristo tunaweza kufikiri ni aina ya kusisimua kuishi maisha ya kutojali. Tunapenda picha ya “Ndio! Ndo mimi huyo! Kuishi bila kujali! “Ni njia maarufu ya kuangalia maisha.

Lakini kwa kusema kweli, Mungu hataki tuishi kwa hali hiyo, kwa sababu ikiwa tunaishi hivyo, basi hatuna nafasi ya kujikinga na makosa.

Barabara zina mistari, moja kwa upande na moja katikati. Mstari huu hutupa nafasi kwa ajili ya usalama wetu wakati tunapoendesha gari. Ikiwa tunapita juu ya mstari upande mmoja, tutaingia shimoni. Ikiwa tunapita kwa le wa katikati, tunaweza kuuawa. Tunapenda mistari hiyo kwa sababu husaidia kutuweka salama.

Ni kama hivyo katika maisha yetu binafsi pia. Wakati tuna mipaka,na vizuizi, tunahisi vizuri zaidi na kushiriki amani ya Mungu.

La muhimu ni kwenda Neno la Mungu, ambalo ameweka mipaka yote tunayohitaji kuishi. Hebu Mungu aongoze njia yako kila siku.


Ombi La Kuanza Siku

Mungu, mimi ninatambua haja ya mipaka katika maisha yangu. Ninaposoma Neno lako, nionyeshe jinsi ya kutumia mipaka yako nzuri katika maisha yangu leo.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon