Mtego wa Kutoshukuru

Mtego wa Kutoshukuru

Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu. WAFILIPI 2:5

Kama binadamu, sisi wote hung’ang’ana na ubinafsi na kukosa shukrani. Tunaweza kuomba na kumwamini Mungu kwa ajili ya kitu fulani, na hata kushukuru sana kwa ajili ya kitu hicho tunapokipokea. Lakini haituchukui muda mrefu sana kabla ya kuacha kushukuru kwa ajili ya kitu hicho na kuanza kufikiri kwamba tuna haki ya kuwa nacho.

Tusipokuwa waangalifu, tunaweza hata kuanza kuwa na nia ya kudai vitu katika uhusiano wetu na Bwana. Tunaweza kuvurugika na kukasirika Bwana anapokosa kutupatia kila kitu tunachofikiri ni haki yetu kupata. Kama watoto wake, tuna urithi kweli, lakini nia nyenyekevu ni muhimu tunapotaka kupokea chochote kutoka kwa Mungu. Nia nyenyekevu humpendeza Mungu na huifanya mioyo yetu ishukuru kwa kila baraka tunayopokea.


Sala ya Shukrani

Baba, ninashukuru sana kwa kazi yako maishani mwangu. Tafadhali nisaidie kuwa na nia nyenyekevu isiyo ya kudai wema wako. Asante kwa kuwa unamimina kibali chako maishani mwangu, sio kwa sababu nimekichuma, lakini kwa sababu tu unanipenda na unataka kunibariki.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon