Mungu hawezi kubadilika, lakini unaweza!

Mungu hawezi kubadilika, lakini unaweza!

Kwa kuwa mimi, Bwana, sina kigeugeu; Malaki 3:6

Kwa nini huwa tunajikuta tukifikiri, Hakuna kitu kitakachobadilika … Mimi daima nitakuwa hivi….. Hali yangu haitakuwa na mabadiliko … Yeye hawezi kubadilika … Yeye hawezi kubadilika … Mimi kamwe siwezi kuwa mzuri kama fulani na fulani?

Jambo pekee ambalo haliwezi kubadilika ni Mungu. Kila kitu kingine kinaweza kubadilika.

Lakini ikiwa huna tumaini la kuona mabadiliko katika hali yako, mabadiliko pengine hayatakuja. Unajua, sisi huvumilia mambo magumu sana amabayo hatufai kuteseka kama tukiweka matumaini yetu kwa Mungu na kuacha kuangalia hali zote ambazo hatuwezi kuzidhibiti.

Hapa ni habari njema: Unaweza kufurahia maisha ikiwa utaamua! Lakini lazima uamini kweli kwamba ni mapenzi ya Mungu kwako uwe na furaha ya daima. Kisha unapaswa kuamua kuingia katika furaha hiyo, ambayo ni muhimu kwa afya yako ya kimwili, ya akili, ya kihisia na ya kiroho. Mungu hubadilika, lakini anaweza kukubadilisha ikiwa unamruhusu.

OMBI LA KUANZA SIKU

Mungu, wakati mwingine ninahisi kama hali zangu hazibadiliki, lakini najua Unaweza kuzibadilisha na Unaweza kunibadilisha mimi. Ninaamua kupokea furaha yako na naamini kwamba utabadilisha maisha yangu.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon