Upendo, Tumaini, na Imani

Upendo, Tumaini, na Imani

Maana katika Kristo Yesu, kutahiriwa hakufai neno, wala kutokutahiriwa bali imani itendayo kazi kwa upendo. —WAGALATIA 5:6

Badala ya kujaribu kwa nguvu kuchochea imani, tutakuwa na hekima tutakapotumia muda na jitihada tu tukipokea Upendo wa Mungu na kumpenda pia. Tutaweza tu kutembea kwa imani kutegemea kile tunachoamini kuhusu upendo wa Baba.

Wagalatia 5:6 inasema imani hutenda kazi kwa upendo. Imani haitafanya kazi bila upendo. Hili linatuambia iwapo hatujui jinsi Mungu anavyotupenda, hatuna la kutegemeza imani yetu.

Kumtumainia Mungu na kutembea kwa imani ni kumwegemea na kumtumainia kwa kila kitu. Unaweza tu kufanya hivyo na mtu ukijua kwamba unapendwa bila masharti. Upendo wa Mungu ni kipawa chake kwetu kisicho na malipo, na tuhitaji tu kukipokea, kushukuru na tukiache kitulete karibu naye.

Biblia inasema, “Tunampenda kwa sababu alitupenda kwanza” (1 Yohana 4:19). Unapokuwa na hakikisho la ukweli kwamba Mungu alikupenda kwanza, utatazamia mbele kumpenda pia—utatazamia mbele kuishi maisha yako kikamilifu kwa ajili yake.

Hakuna mtu ulimwenguni mzima atakayekupenda vile Mungu anavyokupenda.


Imani huwa na nguvu zaidi na kutenda kazi kwa uweza zaidi kwa kuruhusu Mungu kukupenda.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon