vioo vya rangi na vioo vya kukuza

vioo vya rangi na vioo vya kukuza

Kwa hiyo, wewe mtu uwaye yote uhukumuye, huna udhuru; kwa maana katika hayo umhukumuyo mwingine wajihukumu mwenyewe kuwa na hatia; kwa maana wewe uhukumuye unafanya yale yale. Warumi 2:1

Tunapofikiria na kuzungumza juu ya jambo mabaya kwa kila mtu mwingine, kwa kawaida tunadanganywa kuhusu mwenendo wetu. Yesu aliamuru kwamba tusijihusishe na watu wengine wakati tunapokuwa na makosa mengi sisi wenyewe (ona Mathayo 7: 3-5).

Biblia inatuambia wazi kwamba wakati tunapohukumu wengine, sisi mara nyingi tunawahukumu kwa mambo tunayofanya pia! Nilimwuliza Mungu kwa nini tungefanya kitu fulani na kufikiri ilikuwa kikamilifu lakini tuhukumu mtu mwingine ambaye anafanya hivyo.

Bwana alizungumza na moyo wangu, akasema, “Joyce, unajiangalia kwa njia ya kioo cha rangi, lakini unatazama kila mtu kupitia kioo cha kukuza.” Ni kweli! Sisi hutetea tabia zetu wenyewe, lakini wakati mtu mwingine anafanya jambo lile tunalofanya, sisi mara nyingi hatuna huruma.

Ninakuhimiza ugeuze mchakato-ufikie bora zaidi kwa wengine, lakini uendelee maisha yako chini ya kioo cha kukuza. Ruhusu Mungu ashughulike nawe kwanza, na kisha utajifunza njia ya maandiko ya kusaidia wengine kukua.

 OMBI LA KUANZA SIKU

Roho Mtakatifu, badala ya kuchunguza maisha ya wengine, nataka Unisaidie kuchunguza maisha yangu. Najua kwamba kwa msaada wako, ninaweza kusahihisha masuala niliyo nayo na kupata njia nzuri, mwafaka za kuwasaidia wengine kukua pia

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon