Wanyenyekevu hupata msaada

Wanyenyekevu hupata msaada

Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake; 1 Petero 5:6

Kwa kuwa Yesu anatualika tumtwike hofu na wasiwasi yetu, kwa nini wengi wetu tunakataa kumruhusu? Labda hatujui jinsi tunavyoteseka wakati tunapobeba mzigo wa wasiwasi.

Njia pekee ya kuwa na ushindi katika maisha yetu ni kufuata hekima ya Mungu, na anasema tunapaswa kuacha wasiwasi ikiwa tunataka kuwa na amani. Kwa hiyo, wakati mambo yanapojitokeza, tunahitaji msaada wa Mungu. Tunaupataje?

1 Petro 5: 6 inasema kwamba tunahitaji kunyenyekea. Hiyo inaonekana kuwa rahisi sana, lakini wengine wanaendelea kujitahidi wenyewe kwa sababu wao ni wakaidi sana wa kuomba msaada. Lakini wanyenyekevu hupata msaada.

Hivyo kama njia yako haifanyi kazi, kwa nini usijaribu njia ya Mungu? Tunaponyenyekea na kuomba msaada wa Mungu, basi Yeye ana uwezo wa kututolea nguvu zake katika hali zetu. Hiyo basi tunaweza kufurahia maisha. Kwa hiyo nyenyekea leo ​​na umruhusu ashughulikie wasiwasi yako.

OMBI LA KUANZA SIKU

Mungu, najua siwezi kuyatunza maisha yangu kwa amani, na hivyo ninajinyenyekeza leo na kukuombaa msaada. Ninakuamini na kukupa udhibiti katika maisha yangu.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon