Kukaa hatua moja mbele ya shetani

Kukaa hatua moja mbele ya shetani

Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao.  Yakobo 1:12

Ninaamini kuwa kuelewa majaribu na kupinga kwa nguvu ni njia pekee ya kukaa hatua moja mbele ya shetani. Yakobo 1:12  inasema, Heri mtu anayevumilia majaribu … atapata taji la uzima …. Kuvumilia majaribu kunamaanisha kuyapitia majaribu bila kuacha-kwa kumuacha shetani ashinde. Kuvumilia pia inamaanisha kupitiaa wakati wa majaribu bila kuruhusu ibadilishe mtazamo wako au kujitolea kwako. Yesu kamwe hakuwafanyia watu tofauti wakati alijaribiwa, na wakati sisi ni wakomavu wa kiroho, tunaweza kufuata mfano Wake.

Yesu anaelewa hasa kile tunakabiliwa na majaribu. Wakati mwingine anatuwezesha kukabiliana na majaribu ili aweze kuzingatia maeneo ya udhaifu katika maisha yetu na kutusaidia kushinda. Njia pekee ambayo unaweza kuwa nayo yote ambayo Yesu anataka uwe nayo ni kuwa kile alikuumba uwe. Na ukomavu huo unakuja kupitia majaribio.

Kwa hiyo, nuia moyoni kuwa na uvumilivu na kusimama chini ya majaribu kwa neema ya Mungu. Itakuweka hatua moja mbele ya shetani.

OMBI LA KUANZA SIKU

Roho Mtakatifu, naamini wewe uko pamoja nami wakati wa majaribu, hivyo naweza kuwa na subira na kusimama imara, daima kukaa hatua moja mbele ya shetani.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon