Kung’uta Kukataliwa

Kung’uta Kukataliwa

Awasikilizaye ninyi, anisikiliza mimi, naye awakataaye ninyi anikataa mimi; naye anikataaye mimi, amkataa yeye aliyenituma. —LUKA 10:16

Ni ukweli kwamba tutakabiliana na kukatatiwa kutoka wakati moja hadi mwingine. Daudi alikabiliana na kukatawaliwa. Paulo alikabiliana na kukatawaliwa. Hata Yesu alikataliwa. Kwa hivyo ukiteseka kwa kukataliwa kwa sababu ya kufanya kile Mungu amekuongoza kufanya—kufanya vitu ambavyo ni tofauti na vile vitu watu wengine wanafanya—usikate tamaa; uko katika ushirika mzuri.

Mara ya kwanza nilipoanza kuhubiri, sikutosheka na nikawa na kipande changu cha kukosolewa na kukataliwa. Kuna nyakati ambazo nilikataa tamaa kabisa. Mwishowe, Bwana akanena nami katika roho yangu na kusema: “Ni mimi niliyekuita. Usiwe na wasiwasi kuhusu vile watu wanafikiria. Ukifanya hivyo utaendelea kuwa na wasiwasi katika maisha yako kwa sababu shetani hataacha kuinua watu ambao watafikiria mabaya kukuhusu.”

Katika Matendo ya Mitume 28:1–5, Mtume Paulo alipong’atwa na nyoka alimkung’uta nyoka huyo kwa urahisi na hakupata madhara yoyote maovu. Hivyo ndivyo tunavyoweza kufanya na kukataliwa. Tunapomkaribia Mungu na kupata utambulisho wetu ndani yake, badala ya maoni ya watu wengine kutuhusu, tunaweza kukung’uta chochote kinachojaribu kutuvunja moyo. Chochote unachokabiliana nacho leo—hofu, kukataliwa, kukata tamaa, masikitiko, upweke—kung’uta na uendelee na mwendo.


Hata kama kukataliwa kwetu kunatokana na watu walio karibu nasi, tunaweza kuamua kuchuchumilia mbele kutimiza kile Mungu ametuita kufanya.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon