Nguvu ya Kufurahia

Nguvu ya Kufurahia

Furahini katika Bwana siku zote; tena nasema furahini! —WAFILIPI 4:4

Mojawapo ya maagizo mazuri kabisa ambayo Mungu anatupatia katika Neno lake ni kujazwa na furaha na kufurahia. Wazo kubwa lilioje! Hii ni amri ambayo humpendeza Mungu na kuleta faida ya moja kwa moja inayoonekana, ya kihisia na kiroho kwetu tunapofanya hivyo.

Mtume Paulo, kwa kuvutiwa na Roho Mtakatifu, aliwaambia Wafilipi mara mbili kwamba wafurahi. Wakati wowote Bwana akituambia mara mbili tufanye kitu, tunafaa kuwa na hekima ya kuwa wamakinifu na kusikiliza anachosema.

Mara nyingi watu huona au kusikia neno furahi tena na kusema, “Hilo ni zuri, lakini nitafanyaje hilo?” Wangependa kufurahi lakini hawajui vipi! Paulo na Sila, ambao walikuwa wamepigwa, kutupwa gerezani na miguu yao kuwekwa kwa minyororo, walifurahi tu kwa kumwimbia Mungu sifa. Walichagua kufurahi bila kujali hali zao. Walitazamia vitu walivyoamini na sio tu kwa vile ambavyo wangeweza kuona.

Hizo hizo nguvu ambazo zilifungua milango na kuvunja minyororo kutoka kwa Paulo na Sila, na wale wafungwa wengine, zipo leo. Haijalishi unachokabiliana nacho, haijalishi kile wafanyi kazi wenzako wanasema kukuhusu, haijalishi vile watoto wanakusumbua—chukua muda katikati ya fujo hizo ili ufurahi tena. Italeta tofauti!


Kufurahi tena si kitu kinachofanyika kama ajali. Ni uamuzi unaofanywa kwa kufikiri ambao husema, “Nitamsifu Mungu leo, bila kujali hali zinazonizunguka.”

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon