Upendo wa agape wa Mungu

Upendo wa agape wa Mungu

Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. —Yohana 3:16

Biblia inazungumzia aina mbalimbali za upendo. Kuna neno la Kiyunani phileo, ambalo linamaanisha “urafiki au upendo wa huruma.” Kisha kuna eros, ambayo ni upendo wa dhati tunaojisikia kwa mpenzi. Lakini kuna aina ya tatu-aina ya upendo zaidi.

Agape ni aina ya upendo wa Mungu kwa mwanawe na jamii ya binadamu. Ni upendo ambao hutoa dhabihu … upendo tunaoona katika Yohana 3:16: Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu kwa kuwa alitoa Mwana wake peke yake … Kuna maandiko mengi juu ya mada hii; ni kitu ambacho unapaswa kukaa na kujifunza binafsi. Andiko lingine linalofundisha dhana ya upendo wa agape ni Mathayo 5:44. Inatuambia tuwapende adui zetu na kuombea wale wanaotutesa

Si vigumu kuwaombea watu ambao wanatenda mema kwako. Lakini ni vigumu kuombea watu ambao wamekujeruhi. Ni rahisi kushirikiana na marafiki zako kanisani. Lakini ni vigumu kumtafuta mtu huyo anayeonekana kama wa kusikitishwa na peke yake na tumsikilize kwa muda mfupi. Hiyo ni upendo wa agape. Ni sadaka ya faraja yako kufanya haki.

Unawezakuwaonyesha watu “upendo wa agape” kwa kuwa na uvumilivu nao, kwa kuwa na ufahamu pamoja nao, kwa kusema kitu kinachotia moyo au kwa kutosema kitu chochote unapoweza. Kama wanadamu, tuna asili ya ubinafsi, daima tunauliza, “Nitapata nini mimi?” Ni wakati wa kutangaza vita juu ya ubinafsi kwa nguvu ya upendo wa agape.

Ni wakati wa kuwa mzuri na upendo kwa watu kwa madhumuni tunaposoma na kuelewa kile Maandiko inasema kuhusu upendo. Na basi ach upendo wa agape wa Mungu ndani yako uwafikie wengine.


Ombi La Kuanza Siku

Bwana, upendo wako wenye nguvu wa agape ni wa kushangaza. Niwezeshe hata ninapotangaza vita juu ya ubinafsi na kufanya uamuzi kwa kusudi, kuishi maisha ya upendo wa agape.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon