Mungu anaweza kusafisha ufachu wowote

Mungu anaweza kusafisha ufachu wowote

Akini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao. Waebrania 11:6

Nilitendewa vibaya wakati wa utoto wangu. Maisha yangu yalikuwa ya kutisha! Sikumbuka kamwe kuwa na furaha hata nilipokuwa  miaka ishirini. Nia yangu ilikuwa fujo, hisia zangu zilikuwa fujo … kila kitu kilikuwa fujo!

Lakini namshukuru Mungu, sikukaa hivyo! Mungu ameshughulika na mimi, alinibadilisha na kunipitisha katika yote. Sasa nina uhusiano mzuri na Mungu, amani halisi na furaha, uhusiano mzuri na familia na marafiki, na ninafanya kile Mungu ameniita kufanya.

Waebrania 11: 6 inatuambia kwamba Mungu anawapa thawabu wale wanaomtafuta kwa bidii. Nimegundua kuwa kitu chochote nilichotolea sadaka ili nikaribie Mungu na kumtii, nilipokea tena kutoka kwake mara nyingi zaidi. Na kile alinipa mara zote ilikuwa bora zaidi.

Unaweza kuwa unafikiria, lakini Joyce, hujui ni nini ninayohusika nayo. Ni vigumu sana! Ninaelewa-nimepitia mambo mengine ngumu pia. Lakini Mungu atawapa thawabu wale wanaomtafuta. Uwe tayari kumtafuta katikati ya shida yako. Yeye ana uwezo wa kusafisha uchafu wako!

OMBI LA KUANZA SIKU

Mungu, naamini Unaweza kuondoa uchafu wangu. Badala ya kubaki katika shida zangu, ninakutafuta kwa bidii leo na ninatarajia utafanya jambo jema ndani yangu.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon