Shukrani Kila Siku

Shukrani Kila Siku

Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru; nyuani mwake kwa kusifu; mshukuruni, lihimidini jina lake! —ZABURI 100:4

Watu wenye shukrani ni wachangamfu kuwa karibu nao. Kuna watu ambao hupitia katika maisha wakinung’unika, kulalamika, na kukosa shukrani lakini kuna wale pia ambao hupitia katika maisha wakiwa na furaha teletele, wakitazamia mema, kwa wingi wa shukrani. Kwa hakika mimi napendelea kuzungukwa na watu wenye furaha tele, wanaotazamia mema, na wenye shukrani tele—je wewe?

Mioyo yetu ya shukrani tele haitufanyi tu watu ambao wengine watafurahia kutukaribia bali inaonyesha viwango vipya vya ukomavu wa kiroho tunapokuwa na uhusiano wa undani na Mungu. Kadri tunavyomkaribia Mungu, ndivyo tunavyopata kujua zaidi mambo ambayo ametutendea, na kutoa shukrani linakuwa jambo la kawaida kwetu.

Iwapo mtu hana shukrani kwa vitu ambavyo tayari Mungu amempa, kwa nini afikirie kwamba Mungu atampa hata vingine zaidi? Moyo wenye shukrani humwonyesha Mungu kwamba sisi ni wasimamizi wazuri wa kile ambacho ametupatia na kwamba tunaweza kutunza hata baraka zaidi kwa moyo na mawazo yanayofaa.

Wakati ujao ukihisi kutoshukuru, simama na umsifu Mungu kwa kile ambacho tayari amefanya maishani mwako. Hata kama unahisi una kidogo tu, shukuru Mungu kwa kidogo ulicho nacho. Ukifanya hivyo, utashangaa vile atakavyoutuza moyo wako wenye shukrani.


Tazama katika mazingira yako na upate kitu cha kutolea shukrani—uhusiano, mapato, ushindi wa zamani, jibu la maombi. Hakuna kilicho kidogo cha kumsifia Mungu leo!

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon