Tunahitaji Mwelekezi

Kwa maana ndivyo alivyo Mungu, Mungu wetu. Milele na milele yeye ndiye atakayetuongoza (ZABURI 48:14)

Inanifurahisha kujua kwamba Mungu ni mwelekezi wa maisha yetu ya kila siku. Ni ajabu ilioje kujua kwamba kuna mtu wa kutuelekeza na kuhakikisha kwamba tunafika katika mahali pamoja maishani na kwenda pafuatiapo.

Wakati mwingine Dave na mimi tukisafiri, huwa tunakomboa mwelekezi kutonyesha mahali pazuri na muhimu pa kuona. Wakati mmoja tuliamua tutatalii mahali fulani sisi wenyewe; hivyo tukafikiri, tungefanya chochote wakati wowote. Hata hivyo tukagundua kwamba safari yetu tukiwa peke yetu ilikuwa karibu kuharibika. Tulikuwa tukipotea mara nyingi kila siku na kutumia muda mwingi kutafuta njia tena. Tulijifunza kutokana na makosa yetu na sasa tunajua kwamba tunaweza tu kutumia wakati vizuri tukimfuata mwelekezi badala ya kutangatanga ovyoovyo tukitafuta mahali sisi wenyewe.

Ninaamini huu mfano, unaotokana na safari zetu unahusiana na jinsi watu wengi walivyo maishani. Tunataka kujitafutia njia zetu, tuwe waelekezi wetu binafsi na kufanya tunayotaka kufanya wakati ule tunataka kuyafanya. Lakini huwa tunapoteza njia yetu na kuishia kupoteza muda wetu. Mungu ameahidi kutuelekeza katika maisha yetu katika andiko la leo. Hufanya hivi kupitia kwa Roho Mtakatifu, ambaye atazungumza nasi na kutuambia mahali pa kuenda na la kufanya tukimwuliza tu atuongoze.

NENO LA MUNGU KWAKO LEO:

Kila wakati wa maisha yako, hata wa kifo, popote ulipo, Mungu yuko hapo!  

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon