Kuchukua jukumu la furaha yako

Kuchukua jukumu la furaha yako

Mimi najua ya kwamba hakuna jema kwao kupita kufurahi, na kufanya mema maadamu wanaishi. Mhubiri 3:12

 Moja ya masomo muhimu zaidi niliyojifunza ni kwamba siwezi kumtegemea mtu mwingine kunipa furaha. Mungu ametupa uwezo wa kuchukua jukumu la furaha yetu wenyewe.

Watu wengi hawana furaha isipokuwa mtu fulani awe na tabia fulani, au hali fulani ifanye kazi kama vile wanavyotaka. Kila siku tunaruhusu furaha yetu itegemee watu wengine na hali, wakati kwa kweli, Mungu anataka tutafute furaha yetu ndani yake.

Kulikuwa na wakati ambapo ningejisikia huruma ikiwa Dave angeenda kucheza golfu siku moja baada ya mikutano yetu. Nilitaka aende dukani au kuangalia filamu na mimi. Lakini Mungu alinionyeshea kwamba tuna njia tofauti za kufurahi na kupumzika.

Hiyo ni mfano mmoja tu, lakini kuna njia nyingi ambazo tunaweka matarajio yasiyo ya kawaida kwa watu na kuwategemea ili kuendeleza furaha. Mungu anataka tupate kumtazama kwanza na kumtegemea Yeye kwa furaha yetu.

 OMBI LA KUANZA SIKU

Mungu, furaha yangu inapaswa kutegemea wewe tu, sio watu wengine na hali. Nisaidie kuona matarajio yoyote yasiyo ya kweli niliyo nayo ili niweze kuchukua jukumu kwa furaha yangu mwenyewe

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon