Kazi ya Mungu katika Maisha Yako

Kazi ya Mungu katika Maisha Yako

Lakini sisi sote, kwa uso usiotiwa utaji, tukiurudisha utukufu wa wa Bwana, kama vile katika kioo, tunabadilishwa tufanane na mfano uo huo, toka utukufu hata utukufu, kama vile kwa utukufu utokao kwa Bwana, aliye Roho. —2 WAKORINTHO 3:18

Mungu hutubadilisha kutoka utukufu hata utukufu, lakini usisahau kufurahia utukufu ulio ndani yake sasa hivi unapoendelea kwenda kwa unaofuata. Usijilinganishe na watu wengine, au kutathmini kila Mungu anawafanyia kwa kukilinganisha na kile anakufanyia. Kila mmoja wetu ni mtu binafsi, na Mungu hushughulikia kwa utofauti, kulingana na kile anajua tunahitaji.

Huenda usione mabadiliko ya kila siku, lakini ninataka kuchochea imani yako ili uamini kwamba Mungu anafanya kazi, vile alivyosema atafanya. Kumbuka, tunaona baada ya kuamini sio kabla. Tunang’ang’ana kuwa kile tusichokuwa, ilhali tungekuwa tunamsifu na kumwabudu Mungu kwa sababu ya vile tulivyo. Tunamwabudu kwa sababu ya vile alivyo, tunaona vitu vikiachiliwa katika maisha yetu ambavyo hatungefanya vifanyike. Tunapomsifu Mungu, tunawekwa huru kutoka kwa masikitiko. Tunaingia katika utulivu wa Mungu na kuanza kufurahia maisha upya. Kasoro tulizo nazo huanza kupotea na tabia ya Mungu kuachiliwa katika maisha yetu.


Tunaachilia Mungu kufanya kazi katika maisha yetu tunapoendelea kuweka imani yetu ndani yake.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon