Kufanya “vitu vya kawaida” takatifu

Kufanya "vitu vya kawaida" takatifu

Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku, mwingine aona siku zote kuwa sawasawa. Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe.  Warumi 14:5

Kama wanafunzi wa Kristo, tunapaswa kutoa maisha yetu yote kwa Mungu na kumpendeza katika vitu vyote (Wakolosai 1:10). Hata hivyo, sisi hufikiri mambo ya kawaida, majukumu ya kila siku ya maisha kuwa tofauti na mambo mengine ya kiroho ambayo yanatufanya tujisikie haki na Mungu na ni “takatifu.”

Ni lazima tuelewe kwamba, kwa kweli, hakuna tofauti kati ya yale ya kawaida na yale takatifu , isipokuwa katika akili zetu. Kila kitu tunachofanya kinatolewa kwa Bwana; na ikiwa tunafanya kwa moyo safi wa upendo, inakuwa takatifu. Unaweza kufanya kazi za kawaida, kama kwenda kwenye duka la vyakula, na itakuwa takatifu kama sala, kwa kadri unavyofanya yote kwa utukufu na heshima ya Mungu.

Warumi 14 ni sura bora katika Biblia ya kuleta uhuru katika eneo hili. Tafsiri yangu binafsi ya mstari wa 5-6 ni kwamba mtu mmoja anaona sala na kujifunza Biblia kama takatifu kuliko kazi za kawaida, wakati mtu ambaye ni huru kabisa katika Bwana anaona yote ikiwa sawa (takatifu), kwa sababu kila anachofanya, hufanya kwa heshima ya Bwana.

Badala ya kutoa tu sehemu ya maisha yako kwa Mungu, fanya uchaguzi leo kufanya kila kitu unachofanya kitakatifu kwa kumtolea Yeye.

OMBI LA KUANZA SIKU

Mungu, nataka maisha yangu yote kuwa takatifu, si sehemu moja tu. Ninatoa shughuli zangu za kila siku kwako. Ninaishi maisha yangu kukuheshimu.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon