Dhamiri yenye Upole

Dhamiri yenye Upole

Nami ninajizoeza katika neno hili niwe na dhamiri isiyo na hatia mbele za Mungu na mbele ya watu siku zote. —MATENDO YA MITUME 24:16

Njia moja ya kuishi karibu na Mungu ni kuwa moyo wenye upole. Kuwa na dhamiri yenye upole hutuwezesha kuishi karibu na Mungu. Tunakuwa na hisia kwa mguso wake na tunahisi kwa urahisi wakati ule tabia zetu ni sawa au si sawa. Halafu tunaweza kutubu mara moja na kuwa na urejesho upya mzuri wa ushirika na Mungu.

Usiharibu wakati wako kwa kutengeneza visababu vya kukosa utiifu. Mungu anapokuonyesha kwamba umefanya kitu kibaya, sema tu, “Ni kweli, Bwana, nina makosa. Sina kisababu, kwa hivyo tafadhali nisamehe na unisaidie nisirudie tena.”

Ni ajabu vile hilo litakusaidia kudumisha dhamiri yenye upole inayomwelekea Mungu. Tunapokuwa wapole kwa Mungu, inatuwezesha kuwa wapole katika shughuli zetu na watu. Ulimwengu umejaa watu waliotoneshwa, kuumia, na kuvunjika mioyo ambao wanahitaji huruma na mguso wa upendo kutoka kwa Mungu. Acha Mungu awaguse kupitia kwako.


Unapokuwa na moyo wenye upole kwa ulimweleke Mungu, utasikia sauti yake kwa uwazi zaidi na kutii Neno lake kwa utayari zaidi.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon