Kila Wakati

Nitamhimidi Bwana kila wakati, sifa zake zi kinywani mwangu daima. — ZABURI 34:1

Imani na matumaini katika Mungu yanahitaji kufanyiwa mazoezi zaidi ya mara moja baada ya muda au mara kwa mara; tunaweza kuishi katika imani wakati wote. Kwa usaidizi wa Mungu tunaweza kujifunza kuishi kutoka imani hata nyingine, tukimtumainia Mungu mambo yanapokuwa mazuri, na yanapokuwa mabaya. Ni rahisi kumwamini Mungu mambo yanapokuwa mazuri, lakini mambo yakiwa mabaya na tuamue kumwamini Mungu, basi tunakuwa na maadili.

Zaburi 34:1 inatuhimiza kumhimidi Bwana kila wakati. Kuna maandiko mengine mengi yanayotuambia mambo ya kufanya kila wakati—mpinge shetani kila wakati, mwamini Mungu kila wakati, wapende wengine kila wakati—sio tu wakati ambao inakufaa au inapohisi vizuri kufanya hivyo.

Majaribu ni mgeni wa kila wakati katika maisha yetu na mradi tu tuko hapa uliwenguni, tutalazimika kuadhibu hisia zetu, hali zetu, na midomo yetu ili tudumishe uthabiti, utulivu na amani—bila kujali hali na mazingira tuliyomo.

Hilo hutuwezesha kuwa katika ushirika wa karibu na Mungu na kutembea katika furaha ya Roho wake.


Kwa sababu unaweza kuchagua mawazo yako, shaka ikiingia, unaweza kuitambua ni hiyo, na useme, “Hapana, asante,” na uendelee kuamini!

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon