Kumshawishi Mungu au Kumwamini Mungu?

Kumshawishi Mungu au Kumwamini Mungu?

Maana ni nani aliyeijua nia ya Bwana? Au ni nani aliyekuwa mshauri wake? —WARUMI 11:34

Maisha yangekuwa rahisi sana iwapo tungeishi kwa kutambua kwamba Mungu ni mwerevu kutuliko. Hata kama huenda mimi na wewe tutafikiri vipi, njia ya Mungu huwa bora kuliko yetu.

Mara nyingi huwa tunajaribiwa kufikiri tunajua kilicho chema, halafu tunatumia nguvu zetu zote kukifanya kitimie. Mwishowe tunapata masikitiko mengi, ambayo huzuia furaha na raha, kwa sababu ya kujiamulia kwamba lazima kitu kifanyike kwa njia fulani au kwa wakati fulani. Tunapotaka kitu sana, mara nyingi huwa tunajaribu kumshawishi Mungu kuhusu umuhimu wa kitu hicho na kwa nini anafaa kutimiza mapenzi yetu, badala ya kuamini tu kwamba anajua kilicho kizuri kwa maisha yetu.

Vile Warumi 11:34 inavyotukumbusha, Mungu hana haja ya mshauri wa kumwambia kile anafaa kutufanyia. Mapenzi yake timilifu, na ana mipango mizuri juu yetu kuwa yote ambayo anakusudia tuwe. Nabii Yeremia alisema, “Maana ninajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho” (Yeremia 29:11).

Unapokabiliana na hali zinazokanganya, ninakuhimiza kuomba, “Ndiyo Bwana, huenda hili lisilete maana kwangu sasa hivi, lakini ninakutumainia. Ninaamini unanipenda, uko nami, na unafanya kilicho chema kabisa kwa ajili yangu.”


Mungu hahitaji ushauri wako ili afanye kazi; Anahitaji tu imani yako.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon