Kusubiri Vizuri

Kusubiri Vizuri

Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno. WARAKA WA YAKOBO 1:4

Subira ni muhimu sana kwa watu wanaotaka kumtukuza Mungu na kufurahia maisha yao. Tukikosa subira, hali ambazo tunakabiliana nazo maishani zitatufanya kuathirika kihisia.

Wakati ujao ukilazimika kusubiri kitu au mtu, badala ya kukasirika, jaribu kujikumbusha kuwa, kukasirika hakutafanya hili lifanyike haraka, kwa hivyo afadhali nifurahie kusubiri. Halafu pengine sema kwa sauti, “Nimeanza kuwa na subira ninapongoja, kwa hivyo ninashukuru kwa hali hii.” Ukifanya hivyo, utakuwa unatenda neno la Mungu badala ya kukasirika kwa ajili ya hali zisizopendeza. Kumbuka, subira ni tunda la Roho ambalo Mungu anataka kukuza katika maisha yako. Usifikiri tu vile ilivyo ngumu na ya kukatisha tamaa, lakini fikiria kuhusu vile unavyoweza kubarikiwa unapojifunza vizuri sanaa ya kusubiri.


Sala ya Shukrani

Baba, ninashukuru kwamba umepanda subira katika roho yangu na kwamba kupitia kwako, ninaweza kukabiliana na hali yoyote vizuri. Nisaidie leo na kila siku kuwa na subira katika mambo yote.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon