Uzoefu wa Upendo wa Mungu

Uzoefu wa Upendo wa Mungu

Katika hili pendo la Mungu lilionekana kwetu, kwamba Mungu amemtuma Mwanawe pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kwa yeye. —1 YOHANA 4:9

Kwa watu wengi, kama wangeulizwa, “Unapendeka?”—watajifikirisha na kusema, la, sio haswa, sipendeki.

Ninajua huu ni ukweli kwa sababu nilifikiri sikupendeka kabla nije kuelewa jinsi upendo wa Mungu ulivyo na sababu yake ya kunipenda. Hii uelewa wangu usiofaa wa thamani yangu kama mwana wa Mungu uliathiri vile nilivyowatendea wengine. Nilikosa uvumilivu na watu, mkali na mwenye sheria, mwenye kuhukumu, mjeuri, mchoyo na mwenye kutokusamehe.

Mpenyo ulikuja maishani mwangu Mungu alipoanza kunionyesha kwamba sikuwa ninawapenda wengine kwa sababu nilikuwa sijawahi kupokea upendo wake kwangu. Ndiyo nilikuwa nimekubali mafundisho ya Biblia kwamba Mungu alinipenda, lakini sikuwa nimeyakumbatia na kuyapokea kama ukweli katika moyo wangu.

Ukweli ni kwamba huwa inampendeza Mungu kutupenda. Mara unapotambua kwamba unapendwa na Mungu, sio kwa sababu ya kitu umefanya au hujafanya, basi unaweza kuacha kujaribu kustahili upendo wake au kuchuma upendo wake na kuupokea tu na kuufurahia. Hii ni hatua muhimu ya kuishi katika uhusiano wa karibu na Baba.


Sema kwa sauti ya juu mara kumi kila siku, “MUNGU ANANIPENDA!”

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon