Zaidi ya Washindi

Zaidi ya Washindi

Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda. —WARUMI 8:37

Kama waaminio tunaweza kuishi na hisia za ushindi kwa sababu Paulo anatuhakikishia kwamba kupitia kwa Yesu Kristo, tu zaidi ya washindi. Kuamini ukweli huo inatupatia ujasiri wa kuishi kila siku.

Wakati mwingine ujasiri wetu huyumbishwa majaeibu yanapokuja, haswa, yakiwa ya muda mrefu. Lakini tukiwa na hakikisho la upendo wa Mungu juu yetu, haitajalishi kitakachokuja kinyume nasi, tutajua ndani mioyoni mwetu kwamba tuzaidi ya washindi. Kama tuna hakikisho kwa kweli, hatuna haja ya kuogopa matatizo au nyakati za majaribu, kwa sababu tunajua zitapita.

Wakati wowote majaribu ya aina yoyote yanapokuja kinyume nawe, kumbuka kila mara kwamba: Hili pia litapita! Kuwa na hakikisho kwamba katika majaribu hayo, utajifunza kitu ambacho kitakusaidia siku zijazo.

Kadri tulivyo karibu na Mungu, ndivyo tunachukua hatua zaidi za imani, na kuamua kuwa na hakikisho la kitu ndani yake. Watu wenye hakikisho hukamilisha kazi. Wanakuwa wenye kutimilika kwa sababu wanafanikiwa kuwa wao binafsi.


Hatutafanikiwa kuwa sisi binafsi hadi hakikisho letu liwe ndani ya Mungu.

Facebook icon Twitter icon Instagram icon Pinterest icon Google+ icon YouTube icon LinkedIn icon Contact icon